
Sierre - Zinal 2025 Watanzania Hamisi Athumani Misai kutoka Singida na Neema Paulo Sanka kutoka Manyara ni miongoni mwa wanariadha wanaotegemewa kukimbia mbio za Sierre-Zinal nchini Uswisi mwezi wa nane mwaka huu (August 9, 2025) Mbio hizi zimekuwepo kuanzia miaka ya 1970 na kukimbiwa na wanariadha kote duniani isipokuwa kwa nchi yetu ndiyo kwa mara ya kwanza tunawakilishwa na wanariadha hawa wawili. Malengo yalikuwa ni kupeleka wanariadha hadi kumi; kwa maana ya watano wa kike na watano wa kiume, ila kutokana na suala udhamini tumeamua kupeleka hawa wawili kwa kuanza, matarajio ni kwamba mwakani wataongezeka ikiwa wadhamini watajitokeza wa kuweza kupeleka vijana wengi zaidi. Tofauti ya mbio hizi na zingine ni kwamba hizi zinakimbiwa kwenye miinuko ya juu, juu ya vilima vya milima ya Anniviers katika nchi ya Uswisi. Wanariadha hawa wamepata udhamini wa kila kitu kuanzia Usafi ri, Malazi, Chakula, Matibabu, Visa n.k. wakati wa safari yao itakayochukua hadi siku kumi (10) za kukuta...